Recent Posts

JEZI YA BUSUNGU MCHEZAJI WA YANGA YAGOMBANIWA MOROGORO

Malimi-Busungu-1Licha ya matokeo ya ushindi wa Yanga wa magoli 2-0 dhidi ya Mtibwa Sugar magoli yaliyofungwa na Malimi Busungu pamoja na Donald Ngoma na kuvunja mwiko wa kutopata ushindi kwa muda mrefu katika uwanja wa Jamhuri, kuna matukio mengine yalito
kea Morogoro ambayo yalivutia wengi.
Kivutio kikubwa kwenye mchezo huo walikuwa ni mashabiki wa Yanga ambao walikuwa wakisema wamekwenda uwanjani kumshuhudia Malimi Busungu, Amis Tambwe na Thabani Kamusoko.
Lakini hata wafanya biashara wa jezi ambao hukaa nje ya uwanja pindi ambapo Simba au Yanga zinapokuwa zinacheza, nao wamesema kwamba jezi ambazo zilikuwa zikiuzika jana kwenye mchezo kati ya Yanga na Mtibwa ilikuwa ni ya Malimi Busungu ikifuatiwa na Amis Tambwe pamoja na Thaban Kamusoko.
Hata hivyo bado rekodi ya uuzwaji wa jezi ya Jaja iliyowekwa msimu uliopita haikufikiwa, kitu ambacho vilabu vya Tanzania vinatakiwa kujifunza ni kwamba, mbali na kusajili wachezaji ambao wataisaidia timu ndani ya dakika 90, wananafasi kubwa ya kuisaidia timu kuingiza mapato kutokana na kuuza jezi na bidhaa nyingine za klabu kama klabu hizo zitaweka taratibu sahihi.
Simba wamejitahidi kuzindua jezi zao mpya ambazo wanaziuza kwa utaratibu lakini wafanya biashara wengi wa jezi mjini Morogoro jana walionekana wanauza jezi za Simba zamani.
Walipoulizwa kwanini wanauza jezi za zamani wakati tayari klabu hiyo inajezi mpya inazozitumia kwenye msimu huu walisema kwamba, bado klabu hiyo haijaweka utaratibu wa uuzaji wa jezi hizo mpya kwasababu upatikanaji wa faida unakuwa mgumu kwao

No comments