Recent Posts

TAARIFA ZAVUJA HUENDA MOURINHO AKAPEWA MKONO WA KWAHERI, WATAJWA MAKOCHA WATAKAOCHUKUA NAFASI YAKE

Chelsea wanajiandaa kuachana na kocha wa timu hiyo Jose Mourinho kufuatia mwenendo mbovu wa timu hiyo baada ya kichapo cha Jumamosi iliyopita dhidi ya West Ham United.

Kibarua cha Mourinho kipo mikononi mwa bodi ya Chelsea ambao tayari wameanza kumjadili.

Inawezekana kabisa Mourinho akapewa nafasi ya kutetea kibarua chake wakati Chelsea itakapokuwa ikikabiliana na Stoke City kwenye kombe la  Capital One wakati huo kibarua chake kinaweza kuamuliwa na mchezo dhidi ya Liverpool kwenye mechi ya ugenini.

Baada ya kipogo dhidi ya West Ham kwenye uwnja wa Upton Park, Chelsea tayari imeshapoteza michezo sita ya ligi huku ikiwa nafasi ya 15  kwa kuwa na ponti 11.

Kocha wa zamani wa The Blues Carlo Ancelotti anatazamiwa kuchukua mikoba ya Mourinho endapo bosi wa timu hiyo atathibitisha hilo. Lakini pia kocha Guus Hiddink anatazamiwa kuchukua nafasi hiyo kwa muda.

Wakati huohuo Pep Guardiola na Diego Simeone ni majina mengine ambayo ambayo yanatajwa kuchukua nafasi hiyo.

No comments