Recent Posts

THIERRY HENRY AMTAJA MCHEZAJI WAKE BORA WA MUDA WOTE EPL


Gwiji la soka na mchezaji wa zamani wa Arsenal na timu ya taifa ya Ufaransa, Thierry Henry amewashangaza wengi kwa kumtaja kiungo wa zamani wa England na Manchester United, Paul Scholes kuwa ndiye bora amewahi kukutana naye katika historia ya premier league.

Akijibu swali katika interview moja na Sky Sport, alipotakiwa kumtaja mchezaji bora wa muda wote wa ligi kuu England, tofauti na mashabiki wengi ambao wamekua wakiwapa vipaumbele akina Shearer, Henry mwenyewe, Giggs na Cristiano Ronaldo, lakini nahodha huyo wa zamani wa Arsenal amemtaja Paul Scholes kuwa hana mfano wake.

Henry anasema Paul Scholes ndiye mchezaji pekee aliyeweza kuufanya mpira chochote na kwamba kwa mujibu wa Henry, Scholes amekua hapati heshima na sifa anazostahili.

“Paul Scholes ni bora zaidi mimi kuwahi kukutana naye. Timu ya taifa haikutambua ubora wake, lakini Manchester United waliutumia uwezo wake vizuri”.

Xavi Hernandez wa Barcelona anatajwa kuwa ndiye kiungo bora zaidi kwa miaka kumi, aliwahi kusema kuwa kama yeye ni bora kwa miaka kumi, basi Scholes ni kwa miaka 20.

Xavi anasema alikua akiongea na Alonso mara nyingi na kwamba Paul Scholes ni miongoni mwa wachezaji bora zaidi wa kizazi chake. Xavi anasema Scholes anaweza kupiga pasi za goli, ndefu na fupi huku akiwa na uwezo mkubwa sana wa ku-control temper ya mchezo.

No comments