Recent Posts

Kuhusu tetesi za Pogba kwenda Bercelona, Hii hapa ripoti mpya.

Pogba mchezaji mwenye miaka 22 kwa mara nyingine tena amehusishwa kwa kiasi kikubwa kujiunga na club bingwa ya Ulaya Barcelona. Kutokana kiwango kikubwa alichokionyesha kwenye msimu uliopita, kipindi cha usajili kilikua na headline nyingi sana kuhusu Pogba kuhamia Barca.

Muda wa usajili ukapita lakini sasa hivi kuna ripoti mpya kwamba, Juventus wapo tayari kumuuza Pogba lakini wamemuacha acheze kwa msimu mmoja tu wa mwisho.

Habari hizo zimepamba moto na kuchochewa kutokana na kuonekana tri ya Barcelona kutetereka ndio maana anahitajika mtu wa kusaidia kama mmoja wapo akiwa hayupo uwanjani.

Sasa wakala wa Pogba Mino Raiola amejikosea na kuzungumza haya,”Pogba amebaki Juventus kwasababu yeye alipenda kukaa pale kutoka moyoni mwake, kuna ofa nyingi sana zililetwa kwa ajili yake lakini hatukuzipokea.”

Hivyo basi hakuna dalili zozote za kumuona Pogba anacheza kwenye La Liga, lakini ukitaka kumuona huyu jamaa anafanya yake inabidi uwe unacheki Serie A kupitia Startimes live.

No comments